Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Bahá’u’lláh alifunua sala tatu za faradhi, ambazo mojawapo inaweza kuchaguliwa na kila muumini na kuisoma mara moja katika saa 24, kufuatana na maelekezo maalum kwa kila sala. Agizo linalohusiana na sala iliyotolewa hapo chini, ambayo ndiyo fupi kabisa kati ya tatu, ni kwamba ni lazima isemwe mara moja kwa siku kati ya adhuhuri na machweo.
Nashuhudia, Ewe Mungu Wangu, kwamba Wewe Umeniumba, kukujua Wewe na kukuabudu. Nashuhudia katika wakati huu, juu ya unyonge wangu na uwezo Wako, juu ya umaskini wangu na utajiri Wako.
Hakuna Mungu mwingine ila Wewe Msaada katika Mashaka, Aliyepo Mwenyewe.
- Bahá'u'lláh