Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Nimeamka asubuhi hii kwa rehema Yako, Ee Mungu wangu, na nimeacha maskani yangu nikiwa na tumaini kamili Kwako, na nikijiweka katika uangalizi Wako. Nishushie basi, kutoka mbingu ya rehema Yako, baraka kutoka ubavuni Mwako, na Uniwezeshe kurudi maskani mwangu katika usalama kama Ulivyoniwezesha kuondoka nikiwa chini ya ulinzi Wako na mawazo yangu yakiwa yamekaziwa kabisa juu Yako.
Hakuna Mungu mwingine ila Wewe, Mmoja, Asiyelinganishwa, Ajuaye Yote, Mwenye hekima zote.
- Bahá'u'lláh