Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Sifa iwe Kwako, Ee Bwana Mungu wangu! Nakusihi Wewe kwa Ufunuo huu ambao kwao giza limegeuzwa katika mwangaza, kupitia kwake Hekalu liendewalo mara kwa mara limejengwa, na Waraka Ulioandikwa umefunuliwa, na Gombo Lililoenea likafunuliwa, kunitumia mimi pamoja na wao walio wenzangu yale ambayo yatatuwezesha kupaa katika mbingu za utukufu Wako bora kabisa, na yatatutakasa kutokana na madoa ya mashaka kama yale ambayo yamewazuia wasio wanyoofu wasiingie katika hema la umoja Wako.
Mimi ndiye, Ee Bwana wangu, ambaye ameshikilia kwa uthabiti kamba ya wema Wako wa upendo, na nimeshikamana na upindo wa neema na hisani Zako. Niagizie mimi na wale niwapendao, mema ya ulimwengu huu na ulimwengu ujao. Uwape basi, kipaji kilichofichwa ulichoamuru kwa wateule kati ya viumbe Wako.
Hizi ndizo siku, Ee Bwana wangu, ambamo umewaamuru watumishi Wako kuadhimisha mfungo. Amebarikiwa Yule ambaye anaadhimisha mfungo kwa ajili Yako hasa na akiwa amejitenga kabisa na mambo yote ila Wewe. Nisaide mimi na uwasaidie wao, Ee Bwana wangu, kukutii wewe na kushika amri Zako. Wewe, hakika, una uwezo kufanya lolote uchagualo.
Hakuna Mungu ila Wewe, Ajuaye yote, Mwenye hekima zote. Sifa zote ziwe kwa Mungu, Bwana wa malimwengu yote.
- Bahá'u'lláh