Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Utukufu uwe Kwako, Ee Mungu wangu! Hakika mtumishi Wako huyu na mjakazi Wako huyu wamejikusanya chini ya kivuli cha rehema Yako na wameunganika kwa fadhili na ukarimu Wako. Ee Bwana! Wasaidie katika dunia Yako hii na Ufalme Wako na uwachagulie kila jema kupitia Baraka Yako na rehema. Ee Bwana! Wathibitishe katika utumishi Wako na uwasaidie katika huduma Yako. Waache wawe ishara za Jina Lako ulimwenguni Mwako na uwalinde kupitia vipaji Vyako visivyokwisha katika ulimwengu huu na ulimwengu ujao. Ee Bwana! Wanasujudu mbele ya Ufalme wa neema Yako wakiomba mbele ya milki ya umoja Wako. Hakika wameoana katika utiifu kwa amri Yako. Wafanye wawe ishara za utulivu na umoja mpaka mwisho. Hakika Wewe ni Mweza yote, Aliyeko pote, Mwenyezi
- `Abdu'l-Bahá