Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Jina Lako ndilo kuponywa kwangu, Ee Mungu wangu, na kukukumbuka Wewe ni dawa yangu. Kuwa karibu na Wewe ndilo tumaini langu na upendo Kwako ndio mwenzi Wangu. Huruma Yako kwangu ni kiponyesho changu na msaada kwangu katika ulimwengu huu na ulimwengu ujao. Wewe, hakika ni Mwenye Baraka Zote, Ajuaye yote, Mwenye Hekima zote.
- Bahá'u'lláh