Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ee Mungu! Mlee mtoto huyu mchanga katika moyo wa upendo Wako, na umpe maziwa kutoka katika kifua cha Majaliwa Yako. Palilia mche huu mchanga katika bustani ya waridi ya upendo Wako na umsaidie kukua kupitia manyunyu ya baraka Yako. Mfanye mtoto wa Ufalme na umuongoze kwenye milki Yako ya mbinguni. Wewe U mwenye nguvu na mwema, na Wewe U Mpaji, Karimu, Bwana wa Baraka zisizo kifani.
- `Abdu'l-Bahá