Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ee Mungu! Wafundishe watoto hawa. Watoto hawa ni miche ya kiunga Chako cha miti ya matunda, maua ya shamba Lako, waridi ya bustani Yako. Acha mvua Yako iwanyeshee; acha Jua la ukweli liwaangazie na upendo Wako. Acha upendo Wako uwaburudishe ili kwamba waweze kufundishwa, kukua na kuendelea na kuonekana katika uzuri wa juu kabisa. Wewe u Mpaji! Wewe u Mwenye huruma.
- `Abdu'l-Bahá