Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ee Bwana! Mfanye kijana huyu mwangavu na ujalie Baraka Yako juu ya kiumbe huyu mnyonge. Umpe hekima, umjalie nguvu zaidi kwenye kila mapambazuko na umkinge katika kivuli cha ulinzi Wako ili aweze kuondolewa katika makosa, aweze kujiweka katika huduma ya Hoja Yako, aweze kuwaongoza wapotovu, awaachilie mateka na kuwaamsha wazembe, ili wote waweze kubarikiwa kwa kumbukumbu na sifa Yako.
Wewe ndiye Mwenye uwezo na Mwenye nguvu.
- `Abdu'l-Bahá