Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ee Mungu wangu! Ee Ewe msamehe dhambi, Mpaji thawabu, mwondoa huzuni!
Hakika, nakusihi kusamehe dhambi za wale walioacha vazi la kimwili na wamepaa kwenye ulimwengu wa kiroho.
Ee Bwana wangu! Uwatakase kutokana na makosa, ondoa huzuni zao, na ubadilshe giza lao katika mwanga. Wafanye waingie bustani ya furaha, uwatakase kwa maji safi kabisa, na uwajalie waone utukufu Wako kwenye mlima ulio bora kabisa.
- `Abdu'l-Bahá