Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ee Mungu wangu! Ee Mungu wangu! Unganisha mioyo ya watumishi Wako na uwafunulie kusudi Lako lililo kuu. Wafuate amri Zako na kukaa katika sheria Yako Uwasaidie, Ee Mungu katika jitihada yao, na uwape nguvu kukutumikia. Ee Mungu, usiwaache peke yao bali uongoze hatua zao kwa mwanga wa maarifa yako na furahisha mioyo yao kwa upendo Wako. Hakika, Wewe ndiwe Msaidizi na Bwana Wao.
- Bahá'u'lláh