Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ee Bwana wangu, Mpendwa wangu, Haja yangu! Nifanye rafiki katika ukiwa wangu na ufuatane nami katika uhamisho wangu. Ondoa huzuni yangu. Nifanye kujitoa kwa uzuri Wako. Nitoe kwa vyote ila Wewe. Nivutie kupitia manukato Yako ya utakatifu. Nifanye kuwa mshirika katika Ufalme Wako na wale ambao wamejitenga na yote isipokuwa Wewe na wanaotamani kuhudumu katika enzi yako takatifu na wanaosimama kufanya kazi katika Hoja Yako. Uniwezeshe kuwa mmoja wa watumishi wako wa kike ambao wamepata ridhaa Yako njema. Hakika, Wewe ni mwenye Rehema, Karimu.
- `Abdu'l-Bahá