Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Bwana, sisi tu watu wa kuhurumiwa, utupe kibali Chako; tu maskini, utupe fungu kutoka kwa wingi wa ukwasi Wako; tu wenye haja, ututosheleze; tumetahayarishwa, utupe neema Yako. Ndege wa anga na wanyama wa konde wapokea chakula chao kutoka Kwako kila siku na viumbe wote wana ulinzi na upendo Wako.
Usimnyime mnyonge huyu neema Yako ya ajabu na uijalie nafsi hii dhaifu Baraka Yako kwa nguvu zako.
Utupe hakula chetu cha kila siku na utuongezee maisha yetu, ili tusitegemee yeyote ila Wewe, tuzungumze nawe, tutembee katika njia Zako na kutangaza mafumbo Yako. Wewe u Mwenyezi na Mwenye upendo na Mpaji wa wanadamu.
- `Abdu'l-Bahá