Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ee Bwana! Sisi tu wanyonge; tuimarishe. Ee Mungu! Tu wajinga; tufanye wajuzi. Ee Bwana! Tu maskini; tufanye matajiri. Ee Mungu! Tu wafu; tuhuishe. Ee Bwana! Sisi tu fedheha yenyewe; tutukuze katika Ufalme Wako. Ukitusaidia, Ee Bwana, tutakuwa kama nyota zimemetekazo. Usipotusaidia, tutakuwa na hali ya chini kuliko udongo. Ee Bwana! Tuimarishe. Ee Mungu! Tujalie ushindi. Ee Mungu! Tuwezeshe kushinda nafsi na tamaa Ee Bwana! Tuokoe kutoka katika utumwa wa mambo ya kidunia. Ee Bwana! Tuhuishe kupitia pumzi ya Roho Mtakatifu ili tuamke kukutumikia, tujishughulishe katika kukuabudu Wewe na kujibidiisha wenyewe katika ufalme Wako kwa ukweli kabisa. Ee Bwana! U Mwenye nguvu! Ee Mungu, U Msamehevu! Ee Bwana, U Mwenye Rehema!
- `Abdu'l-Bahá