Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ee Mungu, Mungu wangu! Wakinge watumishi Wako waaminifu na maovu ya tamaa walinde na jicho Lako la upendo dhidi ya chuki, karaha ni kijicho, uwahifadhi katika Neno Lako lisilopotoka wawe salama kwa mishale ya mashaka, wafanye wajumbe wa ishara Zako tukufu, ng’arisha nyuso zao kwa miale inayong’aa itokayo katika chimbuko la umoja Wako mtukufu, furahisha mioyo yao kwa maneno yatokayo katika ufalme Wako mtukufu na tia nguvu viuno vyao kwa nguvu itokayo katika milki Yako tukufu. Wewe ni Mwenye Baraka Zote Mlinzi, Mwenyezi na Mwenye rehema.
- `Abdu'l-Bahá