Return to BahaiPrayers.net
Facebook
Ewe Mungu! Ewe Mungu! Huyu ni ndege aliyevunjika mabawa yake na kuruka kwake ni shida sana. Msaidie ili kwamba aweze kuruka kwa upeo wa ufanisi na wokovu, wekelea kuruka kwake kwa furaha kuu na upendo katika nafasi isiyo na kikomo, inua sauti yake katika Jina Lako tukufu ndani ya sehemu zote, changamsha masikio na mwito huu, na ng’arisha macho kwa kutazama dalili za maongozi!
Ewe Bwana! Mimi ni pweke, mmoja na aliye chini. Kwangu mimi sina wa kutegemea ila Wewe, sina wa kunisaidia isipokuwa Wewe na sina wa kunihifadhi kando Yako. Nithibitishe katika kazi yangu, nisaidie na majeshi ya malaika Wako, nifanye mshindi katika kuendeleza neno Lako na uniwezeshe kunena kutoka kwa hekima Yako juu ya viumbe Wako. Hakika Wewe U Mtunza maskini na Mtetezi wa walio wadogo na kweli U Mwenye nguvu, Mwenye uwezo na Asiyeshurutishwa!
- `Abdu'l-Bahá